Mambo yatakayomfanya mwanamke akupende kweli


Katika ulimwengu huu wa mapenzi niliwahi kusikia kuwa ili kumfanya mpenzi wako akuamini sana wewe yapo mambo msingi ambayo unatakiwa kufanyia mwanamke huyo. Pia wataalamu wa mambo wanao msemo wao mtamu usemao mwanamke akipenda huwa kapenda kweli. 

Yafuatayo ndiyo mambo ambayo unapaswa kumfanyia mpenzi wako ili akupende. 

Uwe na muonekano mzuri 
Wanawake wanapenda wanaume wasafi na watanashati kwa hiyo ukiwa msafi na mtanashati utakua na mvuto kwake. Hivyo utakapoamua kumshawishi kufanya mapenzi itakua rahisi yeye kuwa rahisi kukubali. 

Mfanye ajisikie huru 
Ni rahisi mwanamke kufanya mapenzi na mtu anayejisikia huru mbele yake na ambaye yupo huru kuongea na kufanya nae mambo mengine ya kawaida katika maisha. Kwa hiyo ili uweze kumshawishi mwanamke kufanya mapenzi na wewe njia nzuri ni kumfanya ajisikie yupo huru mbele yako na kasha atakua huru kufanya mapenzi na wewe. 

Mfurahishe 
Mfanye ajisikie mwenye furaha kila anapokuwa na wewe na atamani kuwa na wewe. Akishajiskia mwenye furaha kila anapokuwa na wewe ni rahisi kushawishika kuwa na wewe kimapenzi. 

Mfanye ajione kuwa yeye ni mzuri 
Mwanamke anapenda sana na anavutiwa na mwanamme anayeona ubora wake au anayemsifia kuwa ni mzuri. 

Mfanye akuamini 
Mfanye aamini kwamba hata baada ya kufanya mapenzi bado mtakua pamoja na sio mwisho wa mahusiano yenu au urafiki wenu. 

Usiwe na haraka, Mpe muda 
Usiwe na haraka ya kumwambia kuwa unataka kufanya mapenzi na yeye bali subiri mpaka utakapoona yupo tayari au anaelekea kukuhitaji. 

Mfanye akuone mwaminifu 
Mfanye akuone mwaminifu kwa kutomchanganya na wanawake wengine. Usimuonyeshe kuwa una mahusiano na wanawake wengine. Mfanye aamini kuwa unamuhitaji yeye tuu. 

Mjali kama mwanamke 
Mfanye ajiskie kuwa mwanamke. Jaribu kuonyesha kuwa mwelewa, onyesha kuwa unajali, mkarimu na muonyeshe kuwa wewe ni msaada kwake. Mfungulie mlango, mbebee begi au pochi yake n.k. 

Onyesha kuwa unapenda kila kitu kutoka kwake 
Muonyeshe kuwa unampenda yeye na vyote vyake. Onyesha kuwa umevutiwa na yeye na mambo yake yote na sio mwili wake tuu. 

No comments

Powered by Blogger.