Faida za kiafya za asali na mdalasini

 Mchanganyiko wa mdalasini na asali unasaidia katika mambo ya aiana tofauti tofauti kama ifutavto: 

Ugonjwa wa viungo 
Tumia mchanganyiko wa kijiko kimoja cha asali, vijiko viwili vya maji ya ufufutende na kijiko 1 cha mdalasini na upake kwenye sehemu zilizoathirika. 

Kukatika kwa nywele 
Changanya asali, mdalasini na mafuta ya mizeituni kisha upake mchanganyiko huo kichwani na uache kwa dakika 15 kabla ya kuosha nywele zako. 

Kuvu au fungus miguuni 
Changanya kijiko kimoja cha asali, vijiko viwili vya mdalasini na upake kwenye sehemu zilizoathirika usiku kwa muda wa nusu saa, kisha safisha kwa sabuni na maji fufutende. 

Maumivu ya jino 
Changanya vijiko viwili vya asali na kijiko kimoja cha mdalasini na utumia kukupunguzia maumivu ya jino. 

Mafua 
Tumia kijiko kimoja cha asali iliyochanganywa na robo kijiko cha mdalasini, mchanganyiko huu husaidia kuondoa chafya na kuvimba kwa koo. 

Tumbo kusokota 
Asali imetambuliwa kwa kipindi kirefu kwamba ni dawa ifaayo kuondoa kadhia ya tumbo kuchafuka. Unachohitaji kufanya ni kuongeza kiasi kidogo cha mdalasini kwenye asali na uchanganye kisha uongeze maji kikombe kimoja na unywe mchanganyiko huu.

No comments

Powered by Blogger.