Chelsea yaiadhibu Fulham 2-0

Timu ya Chelsea imeweza kurudi kwenye morali ya ushindi baada ya kuibamiza Fulham mabao 2-0 kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya England leo Uwanja wa Stamford Bridge mjini London. 

Magoli ya Chelsea yamefungwa na Pedro dakika ya 4 na jingine limefungwa Ruben Loftus-Cheek dakika ya 82. 

Kwa ushindi huo Chelsea inafikisha pointi 31 baada ya kucheza mechi 14 na kupanda hadi nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England

No comments

Powered by Blogger.