Watu wanaotumia mtandao wa Facebook wazidi kupungua

Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na mtandao wa kijamii wa Facebook idadi ya watu wanaotumia mtandao huo imepungua. 

Kwa mujibu wa shirika la habari la BBC, Facebook imetoa takwimu kuwa watu bilioni 1.49 walitumia mtandao huo mwezi Septemba ikiwa ni chini ya idadi lengwa ya watu billioni 1.51. 

Aidha kiwango cha ukuaji kilipungua zaidi katika mataifa ya Magharibi ambayo ni Marekani, Canada na bara la Ulaya. 

Kwa upande mwingine mtandao huo wa Facebook umeshuhudia ukuaji wa mitandao yake ya kijamii ya WhatsApp na Instagram.

No comments

Powered by Blogger.