Beki wa Simba ahidi makubwa kwa mashabiki

Beki wa timu ya Simba, Shomari Kapombe amewataka mashabiki kutulia kwa kuwa makubwa yanakuja. 

Kapombe ambaye alikuwa kwenye kikosi kilichotwaa ubingwa msimu uliopita alisema kuwa wanatambua kazi kubwa wanayopaswa kufanya kwa sasa ni kupata pointi tatu. 

"Timu inahitaji ushindi katika kila mchezo, tunajua kwamba wapinzani wamejipanga kushindana hilo linatusaidia kujiandaa kuleta ushindani kwenye ligi kwa kuwa tuna kazi ya kutetea taji letu msimu huu. 

Simba wamecheza michezo 10 kwenye ligi kuu  wamefanikiwa kukusanya jumla ya alama 23 wakiwa wamepishana ponti 4 na Azam ambao ni vinara baada ya kucheza michezo 11 wamejikusanyia pointi 27.

No comments

Powered by Blogger.