Kylie Jenner na Travis Scott wanunua Jumba la kifahari la zaidi ya Tsh Billioni 29

Mwanadada Kylie Jenner ambaye pia ni mfanyabiashara aliyejikita kwenye brand yake ya urembo ya ‘Kylie Cosmetics’ na mpenzi wake Rapper Travis Scott wamenunua nyumba ya kifahari inayogharimu zaidi ya Billioni 29 za Kitanzania. 

Inaelezwa kuwa mjengo huo upo maeneo ya Beverly Hills nchini Marekani na kusemekana kuwa nyumba hiyo ilijengwa mwaka 1971 na kuuzwa kwa mara ya mwaka 2012 kwa thamani ya zaidi ya Billioni 13 za Kitanzania na baadae kufanyiwa marekebisho na kurudishwa sokoni mwaka 2017. 

Nyumba hiyo inatajwa kuwa na sehemu nyingi za kuegesha magari, bwawa la kuogelea, vyumba saba vya kulala, master bedroom, jiko, ofisi, chumba cha massage, mabafu 10 na vingine vingi. Inaelezwa kuwa hadi sasa Kylie Jenner tayari ana nyumba tatu. 



No comments

Powered by Blogger.