Jinsi ya kupigilia pamba kijanja

Nimeona leo nitoe darasa kidogo kuhusu mavazi sababu na mimi ni kipaumbele changu katika maisha. 

1.Epuka kuvaa marangirangi 
Wakati unamatch mavazi jitahidi kupunguza idadi ya rangi, rangi 3 tu zinatosha kukutoa bomba. 


2. Vaa kulingana na mazingira/sehemu
Mtu mjanja anajua kubadilika kulingana na mazingira, sio kuvaa jezi la Man utd lenye jina la Wazza kwenye sherehe 



3. Masharti ya kuchomekea 
-Marufuku kuvaa oversize/undersize 
-Usivae mlegezo 
-Hakikisha singlet haionekani 
-Usivae mkanda mrefu 
-Usivae makubanzi/sandals 


4. Kama umevaa pensi /kaptula. 
-Hakikisha unavaa soksi fupi zisizoonekana 
-Piga raba au makubanzi/sandals bila soksi 
-Haipendezi kuchemekea 


5. Usivae shati jeupe kama la mwanafunzi 
Shati nyeupe ni nzuri kama unaijulia wakati unanunua hakikisha ina urembo wa aina yoyote ile au ni ya kimtindo sio kuvaa shati la shule 


6. Hakikisha una suruali nyeusi 
Mwanaume yoyote yule wa kijanja anajua umuhimu wa suruali nyeusi sababu inamatch mashati ya rangi nyingi. 


7. Saa 
-Kama umevaa jeans/kadet unaruhusiwa kuvaa saa ya aina yoyote 
-Kama umevaa suti/suruali ya kitambaa epuka kuvaa saa ya mkanda wa plastic. 


8. Miwani 
Duh hapa pagumu kidogo lakini cha msingi zingatia muundo wa kichwa chako pamoja na aina ya macho uliyonayo na aina ya pamba ulizovaa pia.Sio umepiga jeans kali,kichwa kama madenge na macho kama bundi kisha unapiga miwani ndogo ya njano,ni 




9. Vaa kofia za kijanja 
Kofia pia huongeza mvuto,chagua kofia kulingana na aina ya kichwa na mavazi uliyovaa,haipendezi kuvaa suti na kapelo.Kanzu sharti ivaliwe na barakashia ndo utaeleweka la sivyo ni sawa na kuvaa dera tu 


10. Mkanda 
-Usivae mkanda mrefu km vile umefunga nyoka kiunoni 
-Mikanda ya vitambaa au madoidoi inafaa kuvaliwa na jeans/kadeti/kaptula 
-Jitahidi mkumatch rangi ya mkanda na viatu kama umevaa nguo za kuchomekea 
-Zingatia upana wamkanda na rux za nguo yako 

11.Tupia cheni za ukweli 
Mikufu ya kiume pia huongeza mvuto 
-Kama umevaa nguo za kuchomekea au suti itapendeza ukivaa cheni ndogo ambayo haitokezi nje ya shati 
-Kama umepiga pamba za kishua mfano T.shirt na jeans hapa tupia cheni kubwa lakini hata cheni ndogo zinakubali 


12.Uvaaji wa Tai 
-Vaa kulingana na urefu wako 
-Kama wewe mwembamba inapendeza kuvaa tie nyembamba 
-Jitahidi kumatch tie na rangi ya shirt/suruali 
-Hakikisha tie yako imefungwa vizuri shingoni 


13.T.shirt na Jeans 
Wanaume wajanja wa mjini hupenda kupiga t shirt na jeans na chini kutupia raba Kali.....Vazi hili lina mvuto wa aina yake hasa likivaliwa kitaani na sehemu za mitoko kama vile kwenye Club za starehe. 


14. Vaa viatu kijanja 
Hapa pia Kuna changamoto 
-Usivaa suruali ya kitambaa na Raba 
-Usivae suruali ya kuchomekea na makubanzi 
-Ukipiga jeans unaweza kumatch t.shirt/shirt na rangi ya viatu 
-Ukivaa suti yakupasa upige kiatu kikali ....ulikosea itakuwa sawa na Toyota Mark X yenye matairi ya Fuso !!! 

No comments

Powered by Blogger.