Mambo ya kuzingatia wakati wa kuchagua mpenzi wa kuishi naye

Wakati wa kuchagua mwenzi wako wa kuishi ni lazima uweze kujipanga  katika suala la kufanya maamuzi, hii ni kwa sababu hakuna kazi ngumu hapa duniani kama kuchagua mwenza wa kuishi naye. 

Yafutayo  ndiyo mambo ya msingi ya kuzingatia ili kuchagua mwenzi wa kuishi naye: 

Chagua mtu mwenye huruma. 
Mtu anayeelewa maumivu yako na anayeweza kufanya jitihada za kukuweka sawa pindi unapokuwa katika kipindi kigumu. Chagua mtu mwenye fadhila na mwenye ukarimu; mtu ambaye ana moyo wa huruma, na asiyeogopa kuionesha huruma yake kwa vitendo. 

Chagua mtu ambaye haogopi kufunguka. 
Amini nakuambia, ni jambo salama sana kuwa na mtu asiye na tabia ya kuyaficha maumivu yake moyoni mwake. Na mojawapo ya hali inayoogopesha zaidi katika mapenzi ni ile hali ya kutoweza kujua anachokiwaza mpenzi wako hasa kuhusu wewe. Watu ambao hawako tayari kueleza kinachowasibu au dukuduku zao hujitengenezea bomu la matatizo bila kujijua, bomu ambalo hata lisipolipuka leo linaweza kulipuka muda wowote siku moja bila hata kujua sababu; unaweza kuwa vizuri sana. Naamini umewahi kusikia mikasa ya watu ambao mapenzi yao yaliisha bila ya wao kutarajia, mume au mke anarejea nyumbani kutoka kazini anakuta mwenza wake amekusanya kilicho chake na kuondoka. 

Chagua mtu ambaye anataka kuwa karibu na wewe, kimwili na kihisia. 
Chagua mtu anayependa kuwa karibu kihisia na kimwili; mtu ambaye hachoki kuzungushia mkono wake shingoni, begani, kiunoni au kushikilia mkono wako; mtu ambaye anapenda kukubusu. Kugusa kunaweza kuongeza radha yamapenzi katika uhusiano. Na kwa kuchagua mtu ambaye anaonekana kufurahia kuzungumza na wewe. Mtu ambaye hapendi ujisikie mpweke. 

Chagua mtu ambaye ana maadili mema na mnayeshabihiana. 
Unaweza kupuuzia na kuchukulia kuwa hili ni jambo dogo tena halina maana ya msingi, lakini nakuambia kuwa mtu asiyependezwa na yale unayofurahia anaweza kuishiia kuvuna janga la upweke utakao pelekea kutelekezwa. Na hatimaye wanaweza kumtafuta mtu mwingine ambaye wanaendana naye. Ikiwa wewe ni mkimbiaji, tafuta mkimbiaji; ikiwa wewe ni mwandaaji mziki, tafuta mtu anayevutiwa na muziki; ikiwa wewe ni mtu wa ibada, mtafute mtu anayependa ibada pia!. 

Kufuata ushauri wangu sio njia ya uhakika kwamba hamtatengana. Kwa hakika utakuwa na mambo mengine machache ya kuyazingatia kama; kuwa na tabia njema kwa mpenzi wako, kuwa na heshima, na uwe mwepesi wa kutatua matatizo. 

No comments

Powered by Blogger.