Mpaka sasa Watu 430 wafariki kwa tsunami

Makundi ya uokoaji yanayojaribu kuwatafuta manusura na waathiriwa wa kimbunga cha tsunami kilichoipiga pwani ya Indonesia Jumamosi usiku hatimaye yamefanikiwa kufika katika maeneo ambayo awali haikuwa rahisi kuyafikia licha kutolewa tahadhari. 

Hayo yanajiri wakati idadi ya vifo ikiongezeka na kufika wau tu 430 ambapo Shirika la Kitaifa la Kushughulikia Majanga limesema zaidi ya watu 1,450 walijeruhiwa na 128 bado hawajulikani waliko idadi ambayo pia kwa mujibu vikosi hivyo vya uokoaji inaelezwa kwamba huenda ikaongezeka. 

Aidha inaelezwa kwamba, kufuatia janga hilo la Tsunami watu zaidi ya 11,000 wameachwa bila makazi kutokana na kimbunga hicho ambacho pia kimeharibu miundombinu mingi ya barabara.

No comments

Powered by Blogger.