Ujerumani yatangaza kusitisha kuiuzia silaha Saudia

Jumapili hii Ujerumani imetangaza inaweza kusimamisha kuiuzia silaha Saudia kutokana na kwamba maelezo ya serikali ya Saudia juu ya kifo cha mwanahabari Jamal Khashoggi kuwa ni yenye kutia mashaka. 

Akiongea na wanahabari baada ya mkutano wa chama chake cha CDU mjini Berlin, kansela Angela Merkel alitaka ufafanuzi wa haraka utolewe kuhusiana na kifo cha mwanahabari Khashoggi  na akasema kuhusiana na suala la kuiuzia silaha Saudia, halitafanyika katika mazingira yaliyopo. 

Merkel ilisema aliendelea kufhamisha kuwa  Ujerumani itazungumza na mataifa washirika ili kuchukua maamuzi ya pamoja kuhusu  kifo cha Jamal Khashoggi.

No comments

Powered by Blogger.