Masista watekwa

Masista wanne wa kikatoliki wametekwa nchini Nigeria. 

Ripoti zimeonyesha kuwa masista hao walikuwa wakitoka katika mazishi wakati wanaume wenye silaha walipolivamia gari lao. 

Polisi wa eneo hilo,Mustafa Mustafa amesema kuwa masista hao wametekwa katika mji wa Agbor karibu na reli. 

Operesheni ya kuwasaka watekaji inaendelea. 

Kulingana na vituo vya habari nchini humo,kuna uwezekano kuwa wawili kati ya masita hao walipigwa risasi za miguu wakati wakichukuliwa.

No comments

Powered by Blogger.