Kilimo bora cha korosho

UTANGULIZI 
korosho ni zao ambalo chimbuko lake ni Portuguese na baadae 16 century ndipo lilipo fika africa katika nchi ya mozamboque na baadae likafika Kenya na Tanzania. 
kwa hapa Tanzania korosho ulimwa na kustawi vizuri katika mikoa ya kusini Mtwara, lindi, na maeneo kama Mafia, bagamoyo na Rufiji. 


mvua; korosho ustawi vizuri kwenye maeneo yenye mvua 840mm - 1250 mm wastani wa mvua kwa mwaka, 
napia hukua vizuri kwenye maeneo 0- 500 m kutoka usawa wa bahari. 
udongo; korosho ukua vizuri kwenye maeneo yenye PH 5.6 udongo wa kichanga (sandy) na pia udongo mfinyazi kichanga. 

KUANDAA SHAMBA 
kama mazao mengine shamba la korosho linatakiwa kusafishwa, kusawazishwa nakutifuliwa vizuri kwaajili ya kupanda korosho. 
nakatika mashimo utakayo chimba unaweza kuweka mbolea ya ngombe ukachanganya na udongo mapema ili kuongeza rutuba. 

KUPANDA 
 Ni muhimu sana   kuchagua mbegu bora kwa kua mbegu utakayo panda ndo itakuonesha kiasi gani utavuna, 
baada ya kununua mbegu unachukua maji na chumvi 100g ya chumvi unaweka katika maji kiasi cha lita 5 unakoroga vizuri na unachukua mbegu zako unaweka kwenye maji hayo zile zitakazo zama ndio mbegu zenye uwezekano mkubwa wa kiota, 
 baada ya hapo unazianika vizuri hili ziweze kukauka 
napia unashauriwa kuto panda mbegu zenye umri zaidi ya mwaka mmoja, 
nafasi ya kupanda 12m x 6m kwenye maeneo mvua na kiasi cha miti kitakua 139/hectare 
kwenye maeneo yasio na mvua za kutosha ni 12m x 12m na kiasi cha miti ni 69/ hectare 

MUHIMU 
Kuna aina mbili ya kupanda mbegu ya korosho 
kupanda moja kwa moja; hii ni njia mambayo ni risk sana na inaitaji umakini kwa sababu  kunauweze3kano mkubwa wa mbegu kufa. ukitumia njia hii unatakiwa kupanda mbegu tatu 3 katika shimo moja na baada ya miezi mi 3 - 4 ngoa mimea na bakiza mmoja wenye afya na muonekano mzuri. 
njia ya kitaru; hii ni njia ya pili na ni nzuri kwa sababu unakua huru kuchagua mche ambao umestawi na ulio na muonnekano mzuri , unatakiwa kuamishia miche shambani ikiwa na umri wa wiki 6 na zingatia kuchagua mche wenye afya. 
na baadae unatakiwa kupunguza majani urefu wa sm60- 90 kutoka kwenye ardhi na pia ondoa majani yote ambayo yanaonekana kuadhiliwa na magonjwa au wadudu na yale yalio kauka. 

MAGONJWA NA WADUDU 

MAGONJWA 
Anthracnose 
powdery mildew 
hayo ni magonjwa yanayo athiri thana korosho 

WADUDU 
Cashew stem girdler 
cashew weevil 
coconut bug 
heliotropes bug 
meal bug 
trips aphids 

 KUZUIA NA TIBA 
ili kuzuia maagonjwa na wadudu unatakiwa  
  palilia mapema 
weka shamba katika hali ya usafi 
tumia mbinu ya kuchanganya mazao kwa korosho unaweza kuchanya pamba au maharage hiyo inasaidia kukimbiza wadudu wengine ambao wanakua hawapatani na mazao hayo 
tumia pesticide kutibu magonjwa 
tumia insecticide kuuwa wadudu waalibifu. 

KUVUNA 
Korosho ufikia hatua ya kuzaa matunda pale inapo kua na umri wa miaka 2 1/2 hadi miaka mitatu 
uwezekano wa mkoroso kuishi ni miaka 30 hadi 40 
na kuvuna hua kunaanza mwezi october hadi mwezi december 

MATUMIZI 
chakula 
hutumika kutengeneza rangi 
kama zao la biashara 
miti yake hutumkia kama kuni 
kutengeneza dawa e.t.c 

No comments

Powered by Blogger.